Wanafunzi wa shule ya uoili wakiwa kwenye mahabara. |
Mapendekezo yaliyotolewa na jopo la
kutathmini karo za shule za upili ni mwafaka iwapo yataidhinishwa. Mapendekezo
hayo ya kupunguza karo kwa wanafunzi wa shule za upili za umma yanafaa na ni
afueni kwa wazazi ambao kidogo wamekuwa wakitwika mzigo mkubwa sana wa kulipa
kitita kikubwa cha fedha kila mwaka.
Tume hiyo inayoongozwa na aliyekuwa wazili
wa elimu Dkt Kilemi Mwiria ambaye sasa ni mshauri wa rais kuhusu maswala ya
elimu iliwasilishe ripoti yenye mapendekezo hayo kwa rais ambaye aliyapokea kwa
mwelekeo chanya na kusema kuwa kila motto anapaswa kupata elimu ya kimsingi.
Aidha rais aliongeza kusema kuwa serikali kuu itashirikiana na idara nyingine
pamoja na washikadau husika kuhakikisha kuwa hili litatimia.
Hatua hii itahakikisha kuwa visa vya
wanafunzi kuacha shule kwa ajili ya ukosefu wa karo imezimwa hivyo kwa
wanafunzi ambao huzembea katika masomo yao na kuacha shule hawatawa na sababu
ya kuacha hivyo basi waweza wakachukuliwa hatua za kisheria. Hii pia itatoa
nafasi sawa kwa kila mwanafunzi kupata elimu. Ni matumaini ya kila mzazi kuwa
Rais ataidhinisha mapendekezo hayo baada ya mashauriano na washikadau wote
katika sekta ya elimu.
Mwandishi ni Mburu Samwel
(Chuo Kikuu cha Chuka.)
No comments:
Post a Comment