Wanafunzi wengi hupata furaha
wanapopata fursa ya kujiunga na chuo kikuu. Kwa mfano, nilipopata barua
yangu mwaka wa pili baada ya kuhitimu masomo ya kidato cha nne. Ilikuwa furaha,
shangwe, na nderemo kijijini mwetu kwa kuwa mwana wao alikuwa anajiunga na chuo
kikuu. Chuoni ni mahali ambapo mja akiingia akitoka atatoka akiwa mtu wa
thamani sana katika taifa lake. Ndo maana wote wanafuzu vyuoni huwa nguvu
kazi ya taifa na wanatumiwa kuendeleza uchumi wa dola. Lakini sasa, hiyo sifa imeanza
kufifia na kudidimia. Kwa nini?
Kitambo kidogo, wanafunzi
waliofuzu kwenda chuo kikuu walikuwa wanakaa nje ya chuo kikuu kwa mwaka mmoja
na nusu ivi kabla ya kuingia chuoni. Lakini kutoka mwaka wa 2011, wakati
Naibu wa Rais, Bw. William Ruto alipokuwa Waziri wa Elimu ya Juu,
wanafunzi wamekuwa wakijiunga na vyuo moia kwa moja.
Jambo nzuri lakini kulingana na
wakati huu, naona yapo maafa mengi yanakumba vyuo vikuu. Hawa wanafunzi
wanapata shida ya kudhibiti mhemko na kutoamini kwamba apo vyuoni. Mahali
ambapo pana uhuru wasio kadiria. Uhuru mkubwa kiasi kwamba hamna sare za
kuvalia, kila mmoja ana hiari ya kuvalia gwanda analoliona lamfaa. Ndiposa sasa
tunavyo zungumza, ukipitapita vibarabara vya chuo chochote kile mfano ukiwa
chuo cha Chuka, utatamaushwa na mavazi utakayo yaona. Juzi mzazi mmoja alizirai
alipomwona mwanaye amevalia jinsi hakuwa ametarajia kawe.
Shida nyingine ni ulevi wa pombe na
mihadarati. Kwa miaka nimekwa chuoni mwaka wanne sasa, mwaka huu mambo yamekuwa
makali kuliko miaka yaote. Wanafunzi haswa wa kike wanabugia mvinyo hadharani
bila kujali yeyote wala kuogopa sheria kali za chuo! Zinawafanya mpaka kupigana
kisha kuvunja sheria za chuo. Linalonishangaza ni kwamba hawana habari kwamba hapa
hakuna kutumwa mzazi nymbani! Ole wao kwa sababu wengi wako mbioni kuonana na
jopo la kushughulika nidhamu. Kwani yeyote ambaye amewahi kufika mbelel yake,
adhabu ni kubwa na wengi wao kuivumilia ni shida kwa sababu haistahimiliki
maishani mwao. Lakini lisilo budi hubidi na ukiyavulia nguo lazima uyakoge
ishara ya kukubali adhabu.
Nimeshuhudia mimi wanafunzi
wakipatatna asubuhi mchana wameoana na jioni wanafukuzana kisha kesi naletewa
mimi. Ngono kiholelaholela, na kutofwatilia ule mpangilio uliowekwa ili
kuendesha maisha chuoni. Hili limekuwa likiwapa tumbo joto viongozi wa
wanafunzi vyuoni nikiwa mmoja wao. Haswa idara yangu ikiwa ni ya kushughulikia
maslahi ya wanafunzi chuoni.
Badala ya kusoma, wapo mtandaoni
wakitumia mtandao kuwasiliana, katika mitandao ya kijamii. Maadam tovuti za
ngono zimefungwa, hawangebanduka mle. Mtihani ukifika, baadhi yao wanandika
mpaka ukuta almradi wapite kwa kuwa wakianguka hamna jingine ila kwenda
nyumbani. Ndo sababu ya kufanya lolote kuokoa maisha yake chuoni.
Nimeona uongozi umejaribu kuweka
mikakati ya kukabiliana na haya lakini bado maji yamezidi unga. Ninawaona
washauri nasaha wakiwa mbioni lakini mbio zao ni za sakafuni ambazo mpaka sasa
zinaishia ukingoni. Makundi ya madhehebu mbalimbli mbalimbali chuoni yakijaribu
kuleta msaada. Bado sijaoni dalili ya matumaini lakini lipo tumaini.
Kulingana nami, kuwa katika nafasi
ya kurudisha hadhi ya chuo kikuu, lazima warudishe ule mfumo wa kitambo. Kuokoa
malemgo ya chuo kikuu kisimama imara, sharti serikali irudishe ule mfumo wa
kitambo ili hawa wanafunzi wapate kuona maisha kudogo kabla ya kujiunga na chuo
kwa sababu hilo litafawafanya kubadili msimamo wao kuhusu maisha na kutia
bidii. Na pia kukomaa kidogo.
Pili nimeletewa kesi nyingi sana za
wanafunzi ambao hawana pesa za kuwafanya wawe chuoni. Nikiangalia wale wengi
wanakuja katika hali ya uchochole kwa sababu ya msingi wa familia labda. Lakini
ukiangazia vizuri, huyu mwanafunzi angekubaliwa kukaa nje kwa miaka miwili kama
ilivyokuwa zamani, angetengeneza hela kidogo za kumsaidia kusukuma maisha.
Akifika chuoni, ni kuamsha balaa na belua. Hata kukidhi mahitaji yake ni shida.
Karo nayo ni mlima unaowapa kiwewe kuukwea.
Kwa sasa inabidi ukumbuke
kwamba ile taasisi ya kupoeana mikopo kwa wanafunzi wa vyuo (HELB) pia
haina hela za kutosha kukidhi mahitaji ya wanafunzi wengi wanaongezeka
kila kukicha. Pia taasisi hiyo haina lingine ila kutekeleza amri ya selikali ya
kusema iwape wanavunzi wa vyu anuai mikopo. Usisahau kwamba taasis hiyo pia ina
jukumu la kuwapa mikopo wale wanafunzi wanaosomea ugaibuni. Kinaya ni kwamba
bado hawajaongezewa fedha kutoka hazina kuu ya kitaifa. Ndio maana
tutaendelea kuona migomo ya wanafunzi wa vyuo wakilalamikia ukosefu wa pesa.
Fauka ya hayo, mgaala muue na haki
mpe. Si wanafunzi wote ni watovu wa nidhamu. Wapo wenye maadili. Ukiwaangalia
vizuri unaweza sema wana malezi ya pende mbili. Hao hufanya kile
walinachostahili kufanya na hao ndio hutia for a katika Nyanja mbalimbali ya
kimasomo na hata spoti. Na hao ndiyo kila mtu na hata selikali inajivunia.
Ninapokamilisha ni vizuri kuuliza
swali? Je ni nani anayestahili kulaumiwa ka kupungua nidhamu katika vyuo
vyetu?
Mwandishi ni Frankline Momanyi, Mwanafunzi Chuo Kikkuu cha Chuka.