Sunday 12 October 2014

Uzandiki wa Elimu ya Juu



Kuwa mwanafunzi ni jambo nzuri sana haswa kwa taifa lolote lile kwani linakuwa na matumaini ya kuwa na nguvu kazi ya kutosha kujenga uchumi wa taifa. Ndio maana kila mja sasa yuko mbioni ili angalau kuongeza kitembo chake cha elimu ili kujinyakulia nafasi katika enzi hii ya utandawazi, baada ya wao kubaini ukweli wa msemo usemao ushikwapo shikamana.
Hii inasababishwa na wale wanaosema elimu ni ni mwanga, nami nakubaliana nao mia fil mia. Lakini naomba kuangazia hali ya kuwa mwanafunzi wa chuo kikuu hapa nchini Kenya. Ni jambo nzuri sana kwa kuwa lina haiba yake. Heshima unaporudi kijijini na hata mitaani. Licha ya heshima kuna pia ile kasumba kwamba wanafunzi wa chuo kikuu wana hela kwani wanapewa na selikali. Kinaya.

Nikirejelea maisha ya chuoni, wanafunzi wengi wanasumbuka sana ili kusukuma maisha yao chuoni. ikiwa mwanafunzi anatoka katika familia ya ukabwela, ndiko kuna balaa. Naelewa si mapenzi ya mtu kuzaliwa katika katika familia maskini. Lakini wengine wao wanafunzi wanaotoka lkatika familia maskini, hupatana na maisha ya wenzao ambao wanatoka katika familia tajiri ama kwa jina ingine wenye cheo na mbao si walala hoi.

Unawapata wanaanza hali ya kujiweka katika maisha ya juu ambayo kuyamudu ni lazima ujifunge kibwebwe. Ndo sababu kuu kupata wengine wanapania kujiunga na makundi ya ulanguzi wa mihadarati. Siku hizi wanafunzi wengi  wa jinsia ya kike naya kiume  wote wamekimbila usherati. Na kwa sababu ya utandawazi, wanaweza kwepa kwenda kwenye vijia lakini wanatumia mitandao ya jamii kutafuta shugamummy ama shuga dadi. Hawa ni waume na wake wenye wamea ama kuolewa katika jamii. Wanatafuta hawa wadogo wanaohitaji hela na wao wamalize mahanjam……
Ni vizuri ujue kwamba si wote wanaofanya hivyo kwani kuna wale wanaoshikilia kindakindaki maadili ya jamii. Hongera! Wao hujituma kwa kazi yeyote ile nzuri ili kuunga shilingi moja mbili kwani wanaelewa kwamba haba na haba hujaza kibaba. Wengine wamekuwa machinga. Wao huchuuza vitu hapa na pale ili kutengeneza shilingi.

Najua unajiuliza, mbona wafanye haya yote? Naamini wanafanya haya kwa sababu mahitaji ni mengi na hawana pesa. Ndio maana ubunifu wa kila aina unahitajika ili kuwawezesha kujikimu kimaisha.  Nimeona wengine wakiekeza hela zao kidogo  wanazopata kutoka kwa ruzuku ya selikali. Ni vizuri ufaham kwamba kiwango cha ruzuku hiyo kimepungua kwa kiwango kikubwa. Ndio maana kwa sasa wale wanaopahatika kupata wanapewa shilingi 37,000 badala ya kiwango cha juu cha 60,000. Hili ni jambo la  kutamausha sana lakini kutoka kwa tume hiyo inayopeana ruzuku (HELB) Niliweza kufunga safari mpaka huko ili nijue shida iko wapi. Nilielezwa kwamba hawana hela za kutosha kwa kila mtu kupata kiwango cha juu. Ni heri wapeane kidogokidogo ili wengi wapate.

Wakati mwingi baadhi ya wanafunzi hao hawatambui haya. Ni majuzi tu, tuliona wanafunzi wa chuo kikuu cha Nairobi wakiadamana barabarani wakitaka pesa. Kulingana nami, viongozi wa wanafunzi ndio hutaka tu maandamano hayo kutokea katika taifa letu. Ninaijiuliza tu, Iwapo HELB haina pesa, watatoa wapi kuwapa mkigoma na kuleta hasara yote? Na ilhali hata selikali yenyewe haina pesa inaendelea kukimu mahitaji ya kaunti, ambazo mpaka sasa zinadai kupewa hela zaidi kwa nyimbo zao za pesa mashinani!

Nikichukulia mfano, viongozi wa wanafunzi katika Chuo cha Chuka, mimi nikiwa mmoja wao, sisi tunaelewa shida iko wapi na tunawaita wanafunzi wetu tunawaeleza. Ikibidi kuleta afisa kutoka HELB aje afafanue hayo, tunawaita na wao wako radhi kuitikia wito wetu. Kwa sababu tunaamini katika Nguvu ya majadiliano. Sitasema kwamba hapa chuoni mwetu hamna shida. La hasha! Zipo tena kibao lakini sisi tunazungumza kwenye meza na hili ni jambo nawaomba wanafunzi wote kuiga.
Nikirejerea mada ya ukosefu wa hela, tunaona wanafunzi wengi huwa wanakosa hata uwezo wa kulipa karo. Ndio maana sisi kama viongozi wa wanafunzi Chuka, kuanzisha mpango wa kuwapa wanafunzi wetu ruzuku na wanakuja kulipa baada ya wao kukamilisha masomo yao. Mipango ya kukamilisha hazina hiyo imefika kileleni. Hivi karibuni, hazina hiyo itazinduliwa rasmi. Na naamini itakuwa na uwezo wa kusaidia wengi kulipa karo.

Na wito wangu kwa wanafunzi wote wa chuo kikuu, nyinyi ndio kioo cha jamii. Nyinyi ndio mko katika kilele ya maisha kimasomo. Nawaomba msimame kidete kipigania maadili ya jamii na musiwe ala za kuyavunja. Nidhamu ni chombo imara na hata ukikumbwa na shia gani hata ikiwa ya pesa, jikaze na milango ya kheri itafunguka siku moja. Na muelewe kwamba Rabuka si athmani.

No comments:

Post a Comment