Sunday 27 September 2015
Waumini wazozana kuhusu madai ya ushoga katika kanisa la ACK Nyeri
Hali ya utata inazidi kukumba kanisa la ACK Kagongo katika parokia ya Othaya, kaunti ya Nyeri, baada ya waumini wa kanisa hilo kuandaa misa mbili sambamba wakati mmoja, hii leo katika majengo ya kanisa hilo.
Kundi moja la waumini hao linalomuunga mkono kiongozi wa kanisa hilo, aliyetimuliwa wiki jana pamoja na wengine wanne, kwa madai ya kuhusika katika masuala ya ushoga, lililazimika kujitenga na wenzao waliondaa misa yao ndani ya kanisa hilo.
Sunday 13 September 2015
Wednesday 9 September 2015
OPERESHENI YA KUWAFURUSHA WANAMGAMBO WA ALSHABAAB
ZAIDI YA FAMILIA ELFU MOJA ZIMETOA WITO KWA SERIKALI KUTOWAHAMISHA
KUTOKA KWENYE MAKAAZI YAO YA MUDA MREFU NDANI YA MSITU WA BONI, KATIKA
ENEO LA PANDANGUO KWA KISINGIZIO CHA KUWAFURUSHA WANAMGAMBO WA AL
SHABAAB.
BADALA YAKE WAMEIOMBA SERIKALI KUIMARISHA USALAMA KATIKA ENEO HILO NA
KUHAKIKISHA KUWA CHAKULA KIMEWAFIKIA KWANI NJIA ZA KUJIKIMU
ZIMESAMBARATIKA.
Sunday 6 September 2015
Tume ya kuajiri Walimu yaonya kuwafuta wasiporudi kazini jumatatu
Kufuatia uamuzi uliotolea na mahakamani mnamo tarehe 4 mwezi huu kuhusu
mgomo wa walimu, mwajiri wa waalimu TSC amejitokeza kufafanua uamuzi
huo. Alisema kuwa kulingana naye mgomo huo si halali.
Tume hiyo sasa inawataka walimu wote warudi shuleni kufikia siku ya Jumatatu tarehe saba saa mbili asubuhi.
Aidha tume hiyo iliongezea kuwa wale watakaopuuza agizo hilo basi, hawana budi kutimuliwa kutoka kwa orodha ya waalimu chini.
Saturday 5 September 2015
Subscribe to:
Posts (Atom)