Sunday 27 September 2015

Waumini wazozana kuhusu madai ya ushoga katika kanisa la ACK Nyeri





Hali ya utata inazidi kukumba kanisa la ACK Kagongo katika parokia ya Othaya, kaunti ya Nyeri, baada ya waumini wa kanisa hilo kuandaa misa mbili sambamba wakati mmoja, hii leo katika majengo ya kanisa hilo.
Kundi moja la waumini hao linalomuunga mkono kiongozi wa kanisa hilo, aliyetimuliwa wiki jana pamoja na wengine wanne, kwa madai ya kuhusika katika masuala ya ushoga, lililazimika kujitenga na wenzao waliondaa misa yao ndani ya kanisa hilo.

Wednesday 9 September 2015

OPERESHENI YA KUWAFURUSHA WANAMGAMBO WA ALSHABAAB





ZAIDI YA FAMILIA  ELFU MOJA ZIMETOA WITO KWA SERIKALI KUTOWAHAMISHA

KUTOKA KWENYE MAKAAZI YAO YA MUDA MREFU NDANI YA MSITU WA BONI, KATIKA

ENEO LA PANDANGUO KWA KISINGIZIO CHA KUWAFURUSHA WANAMGAMBO WA AL

SHABAAB.



BADALA YAKE WAMEIOMBA SERIKALI KUIMARISHA USALAMA KATIKA ENEO HILO NA

KUHAKIKISHA KUWA CHAKULA KIMEWAFIKIA KWANI NJIA ZA KUJIKIMU

ZIMESAMBARATIKA.




Sunday 6 September 2015

Tume ya kuajiri Walimu yaonya kuwafuta wasiporudi kazini jumatatu



Kufuatia uamuzi uliotolea na mahakamani mnamo tarehe 4 mwezi huu kuhusu
mgomo wa walimu, mwajiri wa waalimu TSC amejitokeza kufafanua uamuzi
huo. Alisema kuwa kulingana naye mgomo huo si halali.
Tume hiyo sasa inawataka walimu wote warudi shuleni kufikia siku ya Jumatatu tarehe saba saa mbili asubuhi.
Aidha tume hiyo iliongezea kuwa wale watakaopuuza agizo hilo basi, hawana budi kutimuliwa kutoka kwa orodha ya waalimu chini.