Tuesday 8 May 2018

Usichoke Kunipenda by Franklin Pendo


Usichoke kunipenda, Nahitaji mapenzi, makala  Maalum kuhimiza uhusiano Mwema katika jamii.

Usichoke Kunipenda by Franklin Pendo







Usichoke kunipenda, Nahitaji mapenzi, makala  Maalum kuhimiza uhusiano Mwema katika jamii.

GERMS - NO STRINGS in TANZANIAN SWAHILI | Demo





This a Documentary where Franklin Pendo played the role of the Narrator and Character Juma.



Sunday 8 November 2015

Ajali zapokonya maisha wanajamii wakichuma riziki Keumbu, Kisii





Katika bahari ya maisha, kila siku gharama ya maisha inavyozidi kupanda na maisha kuwa magumu, ndivyo wakenya wanavyozidi kukaza kamba katika hatakati ya kutafuta riziki.
Na kwa sababu hii, wananchi katika sehemu ya Keumbu kaunti ya Kisii, wamekuwa wakijihusisha kufanya biashara katika mazingira magumu ambayo wakati mwingine wameshuhudia wenzao wakiaga katika hali ta kuchuma riziki.
Kama anavyotuarifu mwanahabari wetu Franklin Momanyi, kina mama, wana kwa wakubwa huwa wanang'ang'ania mteja wateja katika soko hilo lililo katika barabara kuu ya Kisii Nairobi, huku ikiwawezesha kupata mkate wa kila siku

Ziara ya Papa Francis : Kanisa lachangisha shilingi milioni 124 za maand...



Huku zikiwa zimasalia siku 17 kabla ya Papa Francis kutua humu nchini, shamrashamra za maandalizi zinaendelea kwa kasi, huku kila mdau akijaribu kuhakikisha kuwa mambo yanaenda kama ilivyo pangwa.
Katika kanisa la mtakatifu Paulo Nairobi, waimabaji wanaendelea kupiga msasa, na tumbuizo watakazotumia katika makaribisho ya Papa Nairobi.


Kama mwanahabari wetu Franklin Momanyi anavyotuarifu, haya yanajiri siku moja tu baada ya kuchangishwa shilingi milioni 124.5 katika hafla iliyoongozwa na rais mstaafu Mwai Kibaki, zitakazotumika katika ziara ya Papa humu nchini.

Monday 2 November 2015

Gavana Munya adai wahuni wachochewa na viongozi Meru na Isiolo


Gavana wa Meru Peter Munya ametoa wito kwa serikali kuu kuimarisha  usalama kwa wanachi wa sehemu ya mpaka wa kaunti za  Meru na Isiolo, kufuatia eneo hilo kushuhudia mashambulizi ya mara kwa mara hivi majuzi .

Gavana Munya amesema maswala ya usalama hayajagatuliwa katika katiba  na ni jukumu la serikali kudhibiti hali hiyo kabla haijasambaratika hata zaidi kwani hadi kufikia sasa idadi maasifa wa polisi  katika eneo hilo ni ya chini mno ikilinganishwa na wahalifu wanaoendelea kutekeleza mashambulizi katika eneo hilo

Friday 30 October 2015

KDF washambulia na kuuwa wanamgambo 15 wa Al-shabaab





Kikosi cha wanajeshi wa Kenya chini ya muungano wa Amisom, mapema siku ya Jumapili wamewaangamiza wanamgambo 15 wa Alshabab waliokuwa wakivuka mto Jubba katika eneo la Yantoony kutoka Jilib na kuingia eneo la Juba kusini nchini Somalia.
Kulingana na msemaji wa jeshi la Kenya kanali David Obonyo, shambulizi hilo ni kati ya misururu ya mashambulizi yanayoendelea katika ukanda wa Jubba ili kufanikisha kutwaa eneo la Jilib ambalo ndilo ngome la pekee ya wananamgambo hao kusini mwa Shabelle