Friday 30 October 2015

KDF washambulia na kuuwa wanamgambo 15 wa Al-shabaab





Kikosi cha wanajeshi wa Kenya chini ya muungano wa Amisom, mapema siku ya Jumapili wamewaangamiza wanamgambo 15 wa Alshabab waliokuwa wakivuka mto Jubba katika eneo la Yantoony kutoka Jilib na kuingia eneo la Juba kusini nchini Somalia.
Kulingana na msemaji wa jeshi la Kenya kanali David Obonyo, shambulizi hilo ni kati ya misururu ya mashambulizi yanayoendelea katika ukanda wa Jubba ili kufanikisha kutwaa eneo la Jilib ambalo ndilo ngome la pekee ya wananamgambo hao kusini mwa Shabelle

Saturday 24 October 2015

MOMBASA DISSAPEARANCE MAN

MRADI WA KWANZA WA AINA YAKE WA KUPEANA MAKAAZI YA KISASA

WAUZAJI POMBE HATARI WAVUMBUA MBINU MPYA ZA KUTEKELEZA BIASHA ZAO




BAADA YA MSIMAMO MKALI KUHUSIANA NA BIASHARA YA POMBE HARAMU NCHINI, SASA WAUZAJI WA POMBE HIYO  KATIKA SOKO LA ELDORET KAUNTI YA UASINGISHU, WALIAMUA KUVUMBUA MBINU YA KUWAWEZESHA KUENDESHA BILA KUJULIKANA NA VYOMBO VYA USALAMA KWA MUDA SASA. 

LAKINI LEO SIKU YA ILIKUWA SIKU YA AROBANNE KWA BAADHI YAO BAADA YA WAUZAJI KUMI IKIWEMO BINTI WENYE UMRI MDOGO, KUNASWA WAKIWA KATIKA HARAKATI YA KUWASHUGHULIKIA WATEJA WAO MJINI ELDORET. 

KAMA MWADISHI WETU FRANKLN MOMANYI ANAVYOTUARIFU, WAUZAJI HAO WAMEAMUA KUWEKA HIRIZI KWENYE  MILANGO YAO ILI KUWAOGOFYA ASKARI WATAKAOENDA KUWAKAMATA

Friday 23 October 2015

Familia haijui binti yao yuhai au amekufa mwaka mmoja tangu aliposafiri





Familia moja katika kijiji cha ngamba eneo bunge la Mathioya sasa imekumbumwa na wingu la taharuki baada ya kukosa kujua aliko mwanao ambaye alikuwa akifanya kazi nchini Saudia Arabia.Mary Muringi ambaye kwa sasa amekuwa mfanyakazi wa nyumba nchini Saudi kwa mwaka muda mmoja, alipigia mamake simu na kumtaka kumwombea baada ya kuzuka mtafaruku baina yake na mwajiri wake.
Kuanzia siku hiyo hawajasemezana tena na wala hapatikani kwa simu.

Senata Kiraitu asema angali anafikiria uwezekano wa kusaka ugavana





Seneta wa Meru Kiraitu Murungi ambaye ni kiongozi wa chama cha APK amesema bado angali anafikiria kuhusu iwapo atawainia kiti cha gavana wa kaunti ya Meru katika uchaguzi mkuu wa mwaka wa 2017.
Hii ni kufuatia shinikizo anazopata kutoka kwa viongozi wa sehemu hiyo za kumtaka kumenyana na gavana Peter Munya ambaye kwa sasa, viongozi hao wanasema hawajaridhika na uongozi wake.
Kama anavyotuarifu Franklin Momanyi Munya kwa upande wake anashikilia yuko ngangari kupambana na yeyote yule.

Sunday 18 October 2015

Wazee kutoka Nyeri wafanya tambiko kwa mti kuanguka juma lililopita





Hali ya taharuki imekumba kijiji cha Ngunguru eneo bunge la Mathira kaunti ya Nyeri baada ya mti wa Mugumu, unaokadiriwa kuwa na zaidi ya miaka mia moja kuaguka.
Tukio hili linajiri chini ya saa 48, tangu wazee kutoka jamii hiyo kuzuru eneo la Gamerock kule Nyeri kufanya tambiko kwa ajili ya mti kama huo ulioanguka eneo hilo wiki jana.

Familia haijui binti yao yuhai au amekufa mwaka mmoja tangu aliposafiri



Familia moja katika kijiji cha ngamba eneo bunge la Mathioya sasa imekumbumwa na wingu la taharuki baada ya kukosa kujua aliko mwanao ambaye alikuwa akifanya kazi nchini Saudia Arabia.Mary Muringi ambaye kwa sasa amekuwa mfanyakazi wa nyumba nchini Saudi kwa mwaka muda mmoja, alipigia mamake simu na kumtaka kumwombea baada ya kuzuka mtafaruku baina yake na mwajiri wake.
Kuanzia siku hiyo hawajasemezana tena na wala hapatikani kwa simu.

Saturday 3 October 2015

Meneja wa mikopo Equity auawa, siku moja baada ya zaidi ya sh. milioni 2...





Afisa mmoja anayesimamia mikopo katika makao makuu ya benki ya Equity aliyetekwa nyara na majambazi siku ya Ijumaa usiku, amepatikana amefariki leo asubuhi na mwili wake kuachwa ndani ya
gari lake katika eneo la Redhill huko Limuru.
Kisa hiki kinajiri siku moja tu baada ya wezi waliojidai kuwa wakaguzi
wa vitabu vya hesabu kuzuru benki ya Equity tawi la Othaya jana asubuhi na kuiba zaidi ya shilingi milioni 20.

KUTOKA BAWABU HADI KUMILIKI KAMPUNI!