Sunday 30 August 2015
Rais Kenyatta anunua ngombe kwa sh. 900,000 maonyeshoni Mombasa
Ukistaajabu ya musa, jipange kuona ya firauni! Hii ni baada ya waliodhuria maonyesho ya kilimo mjini Mombasa kubaki vinywa wazi baada ya fahali mmoja kumgharimu rais Uhuru Kenyatta shilingi laki tisa ili kummiliki.
Fahali huyo kutoka ADC Galana ranch, amekabidiwa vijana wa hutuma kwa taifa NYS baada ya rais kumnunua kupitia mnada .
Saturday 29 August 2015
Wednesday 26 August 2015
Monday 24 August 2015
Sunday 23 August 2015
Tuesday 18 August 2015
Ferdinand Waititu Aongoza Wananchi Kuvamia Vilabu Huko Wangige
Hali ya taharuki kutanda katika eneo la Wangige kaunti ya Kiambu, wakati wananchi wa sehemu hiyo walipoamua kuvamia vilabu mbali mbali katika juhudi za kukabiliana na pombe haramu.
Wakiongozwa na mbunge wao Ferdnand Waititu, wenyeji hao walivunja chupa na kumwaga pombe hiyo ambayo walisema imewaathiri vijana katika sehemu hiyo.
Diwani wa zamani adaiwa kuwalawiti wanawe 7,Ruiru
Hali ya mshangao imeghubika kijiji kimoja cha Ruiru baada ya kuibuka madai kuwa mwanaume mmoja mwenye umri wa makamo amekuwa akiwalawiti na kuwabaka wanawe saba kwa muda wa miaka miwili sasa.
Duru za kuaminika zasema kuwa kiongozi huyo wa zamani wa wadi ya Ruiru, amekuwa akiwatendea watoto wake wenye umri wa kati ya miaka miwili na kumi na mitano mtawalia, vitendo vya unyama bila ya mama yao kuwa na habari.
Washukiwa waliokuwa wakielekea Somalia wanaswa Garissa
Watu wawili akiwemo mwanamke mkenya walionaswa na polisi wa kitengo cha kukabiliana na ugaidi, wakiwa safarini kuelekea Somalia,siku ya Ijumaa walifikishwa mahakamani mjini Gararisa.
Inadaiwa mwanamke huyo alidhamiria kuolewa na mwanamgambo wa Al shabaab.
Mlemavu aliyetelekezwa na jamaa zake aamua kuishi mwituni, Meru
Mzee mmoja mwenye umri wa miaka sabini alieamua kutengeneza maskani yake ndani ya msitu, baada ya jamaa zake kumtelekeza katika eneo bunge la Maara, kaunti ya Tharaka Nithi. Mzee huyo licha ya ulemavu wake, amedhihirisha ukakamavu wake katika maisha, kwa kuwa na uwezo wa kutoa ushauri nasaha kwa vijana na hata wazee katika jamii hiyo mwanahabari wetu Franklin Momanyi alimtembelea na kutuandalia taarifa ifuatayo.
Mambo unayofaa kuzingatia unapoogelea baharini, ziwani au mtoni
Ni msimu wa likizo wakati ambapo watu wengi hupendelea kutafuta mahali pa kujivinjari na kuondoa msongo wa panda shuka za maisha.
Wana kwa watu wazima aghalabu huelekea Pwani angalau kuogelea na kubarizi kwenye mchanga wa baharini.
Lakini la kutamausha ni kwamba wapo wengi ambao wamekumbwa na majanga makubwa katika harakati hizo kwa mfano, visa vya hivi punde vya kufa maji kwa wanafunzi saba baharini na kuzama kwa wavuvi watatu katika ziwa Naivasha.
Franklin Momanyi anaangazia tahadhari zinazofaa kuchukulia kabla ya kuanza mtu kujitosa majini kuogelea.
Subscribe to:
Posts (Atom)