Sunday 8 November 2015

Ajali zapokonya maisha wanajamii wakichuma riziki Keumbu, Kisii





Katika bahari ya maisha, kila siku gharama ya maisha inavyozidi kupanda na maisha kuwa magumu, ndivyo wakenya wanavyozidi kukaza kamba katika hatakati ya kutafuta riziki.
Na kwa sababu hii, wananchi katika sehemu ya Keumbu kaunti ya Kisii, wamekuwa wakijihusisha kufanya biashara katika mazingira magumu ambayo wakati mwingine wameshuhudia wenzao wakiaga katika hali ta kuchuma riziki.
Kama anavyotuarifu mwanahabari wetu Franklin Momanyi, kina mama, wana kwa wakubwa huwa wanang'ang'ania mteja wateja katika soko hilo lililo katika barabara kuu ya Kisii Nairobi, huku ikiwawezesha kupata mkate wa kila siku

No comments:

Post a Comment