Monday 2 November 2015

Gavana Munya adai wahuni wachochewa na viongozi Meru na Isiolo


Gavana wa Meru Peter Munya ametoa wito kwa serikali kuu kuimarisha  usalama kwa wanachi wa sehemu ya mpaka wa kaunti za  Meru na Isiolo, kufuatia eneo hilo kushuhudia mashambulizi ya mara kwa mara hivi majuzi .

Gavana Munya amesema maswala ya usalama hayajagatuliwa katika katiba  na ni jukumu la serikali kudhibiti hali hiyo kabla haijasambaratika hata zaidi kwani hadi kufikia sasa idadi maasifa wa polisi  katika eneo hilo ni ya chini mno ikilinganishwa na wahalifu wanaoendelea kutekeleza mashambulizi katika eneo hilo

No comments:

Post a Comment