Sunday 19 October 2014

WASOMI WANAOENEZA UKABILA WANA MENGI YA KUSOMA KUTOKA KWA PROF MAZRUI.



Top of Form
Bottom of Form
Prof. Mazrui

Kifo chake Prof. Mazrui si pigo tu kwa Kenya bali ni kwa ulimwengu mzima. Alikuwa mmoja kati ya watu ambao kuchezea kwenye kiwango chake ilikuwa vigumu. Kwa kweli Profesa Mazrui alikuwa vitu vingi vilivyowekwa ndani ya mtu mmoja. Hakuwa tu msomi mtajika balialikuwa shupavu wa kutetea haki za kibinadamu mwandishi aliyekamilika na pia mchanganuzi wa maswala ya kisiasa.
Wakati ambapo wenzake walieneza chuki za kikabila na tofauti za kidini yeye hakutawaliwa na mambo madogo kama hayo. Yeye alishughulika na maswala ya kuelimisha ulimwengu kwa kusimama kidete kutetea haki za wanyonge na waliotelekezwa mahali popote walipokuwa ulimwenguni. Wakati ambapo wataalamu wengi waliogopa kukashifu uongozi wa kiimla yeye alisimama wakati mmoja na kuingilia uongozi wa KANU na hili likasababisha yeye kunyimwa kazi ya uhadhiri katika chuo kikuu cha Nairobi. Mageuzi mengi Kenya yalifaidi kutokana kwa mchango wake adhimu.
Yeye alitupilia mbali dhana ambayo ilikuwepo kwamba dini ya kiislamu ilikuwa ya vita tu. Hata baada ya mataifa ya magharibi waliobuni uvumi kuhusu uislamu yeye hakusikia hata bali alishikilia msimamo wake kwamba dini hiyo si ya kivita wala zogo la kila wakati. Kwenye maswala ya kiakademia alichangia pakubwa katika taaluma ya usomi kupitia kazi zake aula. Ni aibu kubwa katika karne hii kuona wasomi wengi wakitawaliwa na ubarakala na ukabila jambo ambalo ni tisho kwa utaifa. Swali langu ni je mbona tuwe na wasomi wengi ambao watawa wasumbufu kwa ajili ya chuki za kikabila? Kila wakati usomapo makala unaweza ukatathmini mwandishi ametoka kwenye kabila lipi.
Hakuchoka kuandika maswala ambayo ylisumbua bara la Afrika na watu wake. Wakenya wanaweza kufuata na kumheshimu profesa Mazrui kwa kuzingatia na kufuata katiba ilivyo kwa kikamilifu. Roho yake na iwatie motisha wengi wanaopania kuwa wasomi halisi wasiojikita katika maswala ya ukabila, ubarakala na ubinafsi. Lala salama mtetezi wa haki za kinadamu na msomi mtajika.

Mwandishi: MBURU SAMWEL.

No comments:

Post a Comment