Thursday 16 October 2014

Wachuuzi waumia Nairobi



Ni jambo la kutamausha kuona yale yanayowasibu wachuuzi katika jiji la Nairobi. Ni dhuluma kwa kaka na dada zetu wakenya wanaojitahidi kutafuta cha kutia mdomoni. Lakini sasa kuwa machinga limekuwa ni jambo ambalo si la kuvutia Miongoni mwa wakaazi wa jiji la Nairobi. Mbona kusumbuliwa na kufanyiwa madhila yote na wao wanajitafutia cha halali? Kweli myonge hana haki.

Inauma kuona zile hela umewekeza katika katika biashara yako kama mtaji ikigeuzwa jivu na askari ambao wanafaa kukutetea wewe kama mlipa ushuru. Askari wa kaunti wamekuwa wakiwadhulum machinga wa jiji la Nairobi haswa pale ngara, na eneo la globe cinema. Wanawake wakishikwa wanaweke wakikamatwa, ni kunyanganywa hela zao, wengine wanavuliwa nguo zao na hata kubakwa ndani ya magari yao. Na waume nao wakishikwa, wananyanganywa hela zao na kuchomwa visu licha ya kupokea kichapo cha mbwa mskitini.

Swali langu ni kwamba mbona wawe wanawadhulum na kuwapiga vile? Najua utasema kwamba kuna sababu. Kulingana na vile nimeona wakifanya, askari wa jiji wanawafukuza kutoka eneo la fig tree kwa madai kwamba wanataka kujenga bustani, mara stendi ya basi, mpaka sasa hawajapewa mahali pa kwenda. Mimi naelewa ukifukuza mtu atoke mahali anafanyia biashara yake, basi mpe mahali mbadala ya kufanyia kazi yake.
Wachuuzi wa soko wakitoroka askari wa kaunti ya Nairobi katika eneo la Globe Cinema.
Kuchukuwa mali yake na kugawana yanayobaki mnachoma si jambo la halali. Na jambo la kukeketa maini ni kwamba askari wa taifa huwa wako pale wanaangalia tu. Mchuuzi akiumizwa aende kupiga ripoti mara nyingi wanasema “ni bahati hawakukuuwa” na hawa askari wamekula kiapo cha utumishi kwa wote! Kinaya
Na kulingana na ripoti ya viongozi wa kaunti ya Nairobi, wao wamesema hawajui kama swala hilo lipo. Lakini itakuwaje wakenya walipa ushuru kuumizwa kiasi kile na mseme hamjui? Swali linguine naulizwa kwani wale nanaotetea haki za binadam, wako wapi kutetea hawa machinga? Ama jambo linakuwa la kukiuka hali za kibinadam wakati bwenyeye amekosewa na wakati mtu wa kawaida amekosewa sio jambo la haki za kibinadamu?

Ni vizuri kuonyesha kwamba,  ndio wachuuzi hao huwa na hulka mbaya, hulka ya kutumia nguvu. Hulka ya kuwafanya askari wa jiji watumie silaha  butu ili kujaribu kuleta nidhamu lakini mbona kujinyakulia haki mkononi? Tangu lini mtu akatiwa nidhamu kwa kuchomwa kisu? Mimi naelewa ipo sababu ya haya kutokea. Baadhi ya askari wengi wa kaunti ya Nairobi huwa wanataka kitu kidogo na iwapo mchuuzi hayupo radhi kumpa basi wananyakua bidhaa zake na kuchukuwa ama wanachoma mchuuzi akiangalia. Na jambo hili linawafanya wawe na mawazo hasi haswa yanayo wafanya wawe wakivunja sheria zilizoko kwa machungu ya kudhulumiwa. Ikiwa mtu amekosea, mshike na ushahidi kisha mpeleke mahakamani ahukumiwe kulingana na mujibu wa sheria.

Mimi naomba selikali kuu iingilie swala hili kuwasaidia wakenya wanaojitetea kutafuta riziki. Pia selikali ya kaunti kuketi chini na viongozi wa wachuuzi ili kutafuta suluhu kwa jambo hili. Pili lile kundi la kutetea haki za kibidamu liingilie kati. Lakini ni muhimu kuzingatia maridhiano baina ya pande zote mbili ndilo jibu tu la tatizo hili.

No comments:

Post a Comment