Wednesday 22 October 2014

Sepetuko la mapenzi



Ni jambo la kuudhi sana kumwona mtu akidondokwa na machozi kwa kuachwa na mpenzi wake miezi michache tu baada ya kuanzisha uhusiano. Wengi hulia, hupoteza mwelekeo huku wengine wakijitia kitanzi baada ya tukio hili kutokea. Naomba  tulitathmini swala hili kwa kifupi. Iwapo mpenzi wako  amefariki, je, utaishi maisha ya ukapera milele? Iwapo  umegundua kwamba mpenzi wako si mwaminifu kwako, utahisi vipi? Mnapokuwa katika uhusiano wa mbali, yepi huibuka?

Asilimia kubwa ya walio kwenye uhusiano wowote wa kimapenzi, hutafuta mpenzi mwingine pindi tu mwenzi wao dhati wanapoelekea jongomeo. Wengi hudai kuwa ni njia ya kuponya vidonda huku idadi ama asilimia ndogo wakibaki kapera. Na wanapogundua kuwa wapenzi wao si waaminifu kwao na kuwa wanajihuzisha na ‘mpango wa kando’ hujitia kwenye uwanja na kutafuta mipango yao ya kando, bila kujali madhara kama, magonjwa ya zinaa huenea kuingia  kwenye familia.

Wengi kati ya wale ambao wako na uhusiano wa  mbali hufeli kwani wapenzi hukosa wakati tosha wa kuwa pamoja ili kusemezana na kujuliana hali. Hufika wakati ambapo kidosho hataki mwanamume na kwa sababu mpenzi wake yuko mbali humlazimu kutafuta wa karibu ambaye watakuwa wakionana mara nyingi. Ni wachache ambao huweza kusimamisha uhusiano wa mbali hasa walio na uwezo wa kutembeleana mara nyingi kwani hili huchangia sana katika kukuza uhusiano.

Ni bayana kuwa ‘Upendo haudumu’ kwani mtu huweza kumsahau mpenzi wake na kumchukua mwingine na hili laweza jirudia mara kwa mara. Sioni sababu mwafaka ya kusema umempenda mtu kwani kila siku, kila dakika binadamu hupendezwa na anachokiona.‘Upendo au undani ni jambo la kuwaza na sioni haja ya kulia unapoachwa na mpenzio. Ninaloliamini ni kuwa hakuna ‘mapenzi’. Hayo ni madai ya kiakili tu. Huwezi pendezwa na mwingine iwapo unampenda uliye naye.



Mwandishi: BENSON WAWERU, Chuo Kikuu cha Chuka
 

No comments:

Post a Comment